Tuesday 7 May 2013

(TAMKO LA BAKWATA) TAARIFA KWAVYOMBO VYA HABARI TAMKO LA BARAZA KUU LA WAISLAMU WA TANZANIA BAKWATA JUU YA MLIPUKO WA BOMU - ARUSHA

Assalaam alaykum warahmatullahi wabarakaatuh. ... Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania BAKWATA, limepokea kwamasikitiko makubwa tukio la kurushwa bomu Kanisani na kusababisha upotevu wa maisha na majeraha kwa watu wengi wakati wa sherehe ya uzinduzi wa jengo la Kanisa la Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Orasiti, Arusha. Kimsingi hili ni jambo la kusikitisha,kukera na kufadhaisha sana kutokea hapa nchini. Watanzania kwa miaka mingi, tumezoea hali ya utulivu na amani na tukio kama hili ni changamoto kwa usalama wa Watanzania wote nchinzima Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania BAKWATA linalaani kitendo hicho cha kikatili na inaviomba vyombo vya dola kufanya jitihada zote kuhakikishawahusika wanakamatwa na wanachukuliwa hatua, kwani msiba huu ni wetu sote, Wakristo na Watanzania wote. Kwa niaba ya Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania mimi SheikhIssa Bin Shaaban Simba Mufti wa Tanzania nawapa pole wafiwa wote katika tukio hilo na kuwaombea dua majeruhi na Mwenyezi Mungu (SW) awape tahfif na wapone haraka na kurudi katika shughuli zao za kila siku. Wabillahi Tawfiiq. SHEIKH ISSA BIN SHAABAN SIMBA. MUFTI NA SHEIKH MKUU WA TANZANIA BARA.

No comments:

Post a Comment