Thursday 9 May 2013

WAYNE ROONEY AOMBA KUONDOKA OLD TRAFFORD

Uongozi wa United wameshikwa na butwaa kufuatia straika wakeWayne Rooney kuomba kuondoka klabuni hapo. masaa manne kabla Sir Alex Ferguson hajauthibitishi a uongozi wa juu wa klabu hiyo kuhusu kuachia ngazi kwake kama meneja wa United mwishoni mwa msimu huu, kumpisha meneja wa sasa wa klabu ya Everton David Moyes kushika hatamu, Sportsmail wametanabaisha kwamba Rooney alimwambia Ferguson wiki mbili zilizopita anataka kuanza upya. Kama Rooney atabakia klabuni hapo na Moyes kushika wadhifa huo utakaoachwa na Ferguson basi atapata fursa ya kufanya kazi tena na bosi wake wa kwanza Moyes - ambaye anatarajiwa kuthibitishwa muda wowote leo. Akiwa anakasirishwa na yanayomtokea hapo klabuni, Rooney na Ferguson wakiwa kwenye hicho kikao katika ofisi zameneja huyo kua ni bora aachwe aondoke pindi dirisha la usajili litakapofunguli wa mwezi wa saba. Taarifa zinaendelea kudai kwambaFerguson, alimwambia kwa kufuatia hawezi kumthibitishia kumuuza ama kutokumuuza. Rooney kwa sasa atafikiria upya kua chini ya kocha wake huyo wazamani Moyes, ingawa hapa kipindi cha nyuma wameshasemeana mbovu. Bado inasubiriwa kuona kwamba baada ya maongezi kama Rooney atashupalia suala hilo na kuiandika barua rasmi ya kutaka kuondoka klabuni hapo. Rooney anajua kwamba Chelsea wako tayari kumchukua muda wowote kujiuga Stamford Bridge, ilhali Bayern Munich na Paris Saint-Germain nao pia wangependa kufanya nae kazi. Haya kama shabiki wa Chelsea ungependa kumuona Rooney Stamford Bridge? Mpenzi a Man U - ungefurahia abaki ama aondoke tu. Kazi ni kwako mwanamichezo wa The Tz.

No comments:

Post a Comment