Zanzibar. Katibu Mkuu wa Chama Cha
Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema hajaridhishwa na rasimu
ya kwanza iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na
Jaji Joseph Warioba.
Kauli hiyo aliitoa wakati akihutubia maelfu ya
wafuasi wa chama chake katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika
Uwanja wa Tundangaya Matemwe iliyoko Wilaya Kaskazini ”A’ Unguja.
Alisema chama chake kimeunda jopo la wanasheria
weledi kwa lengo la kuipitia na kuichambua kifungu baada ya kifungu ili
kutoa ushauri kuhusu rasimu hiyo.
“Rasimu hiyo mimi sikuridhika nayo tumeiona na
tumeipitia na tumeunda jopo la wanasheria ili watushauri,” alisema
Maalim Seif huku akishangiliwa na wanachama wake.
Alibainisha kuwa kuna mambo ambayo yalitakiwa
yatolewe katika mambo ya Muungano ndani ya rasimu hiyo ambayo yangetoa
mamlaka kamili ya Zanzibar bado yamebakishwa yakiwa ni mambo ya
Muungano.
Mambo hayo ni kama ulinzi na usalama, sarafu na
Benki Kuu, mambo ya nje ,usajili wa vyama vya siasa ushuru wa forodha na
mapato yasio ya kodi yatokanayo na mambo ya muungano
Alisema kwa Zanzibar kwa yale mambo ambayo si ya Muungano wataweza kushirikiana na nchi yoyote ile duniani.
Alisema kuna baadhi ya mambo walitaka kuwamo ndani
ya rasimu ya Katiba Mpya kuna baadhi ya mambo hayo yamo na mengine
hayamo kabisa lakini mengine hayamo na mengine yamo nusu.
Hata hivo akizungumzia suala la kujiandikisha
katika daftari la kudumu la wapiga kura alisema ili uweze kutoa uamuzi
wa nchi yako lazima uwemo katika daftari la wapiga kura la Wazanzibari
kama humo huwezi kupiga kura.
Alimtaka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Jecha
Bakari Jecha kuwa tume yake ni mpya tayari imepanga mikakati ya
kuwakosesha wananchi kujiandikisha kwa kutumia mawakala au sheha
akimkataa tu mtu basi asiandikishwe.
No comments:
Post a Comment